Header Ads

MARK ZUCKERBERG ;- AKIWA ANAKULA UGALI NA SATO NDANI YA KENYA

Ukiwa bilionea, tena unayemiliki app zenye nguvu duniani, Facebook, Instagram na Whatsapp si rahisi watu kukufikiria iwapo unaweza kula chakula cha Kiafrika.
Kwa Mark Zuckerberg, CEO wa Facebook maisha rahisi ni kitu anachopenda licha ya kuwa na utajiri unaokadiriwa kufika dola bilioni 40.
Bilionea huyo wa Marekani alikuwa Kenya wiki hii kwenye ziara yake ya kwanza Afrika akitokea Nigeria na kujumuika na wenyeji wake kula ugali na sato – bila kusahau sukuma wiki pembeni.
Zuckerberg anakutana na wajasiriamali kwenye teknolojia na kutembelea vituo vya ubunifu katika sekta hiyo.

No comments

YoungGskillz.com . Powered by Blogger.